Pia inasemwa kwamba Moyes hajawahi kusafiri na timu kwenda hata jijini Milan kutetea ushindi. Zaidi ya yote, Moyes si kama Jose Mourinho.Akiwa kocha wa Everton, staili yake ya uchezeshaji ni nzuri lakini haihamasishi kusaka ubingwa.
WIKI hii kumekuwa na mlolongo wa matukio kwenye soka la
kimataifa. Jumatano kocha, Alex Ferguson, alitangaza kujiuzulu na juzi
Alhamisi kocha wa Everton, David Moyes, alipewa mikoba ya kuiongoza
Manchester United.
Ferguson anasema kocha huyo ni mzuri na
ataifikisha timu mbali, lakini wengi wanajiuliza iwapo Moyes ni thabiti
kuongoza klabu hiyo na kama anaweza kupata mafanikio ya kocha huyo
kutoka Scotland.
Kuna taarifa mbalimbali zinazosema kuwa Moyes hana
sifa ya kuwa kocha wa Manchester United, kila mmoja anatoa sababu
zake.Kinachoelezwa kwa Moyes ni kwamba, hakuwahi kutwaa vikombe wala
kufundisha timu iliyowahi kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Hakuwahi kumnasa mchezaji wa dau linalofikia Pauni
30 milioni, hafahamu mipango ya kutengeneza mazingira ya kutwaa ubingwa
katika hatua za mwisho wa ligi.
Pia inasemwa kwamba Moyes hajawahi kusafiri na
timu kwenda hata jijini Milan kutetea ushindi. Zaidi ya yote, Moyes si
kama Jose Mourinho.Akiwa kocha wa Everton, staili yake ya uchezeshaji ni
nzuri lakini haihamasishi kusaka ubingwa.
Itakumbukwa katika msimu ambao Blackpool ilicheza
kabla ya kushuka daraja, iliifunga Everton na kikosi cha Moyes
kikamaliza nafasi ya saba.Kwa upande mwingine, Manchester United chini
ya Sir Alex Ferguson ina kazi ya kusaka mabao tu. Katika misimu minane
ya Moyes, nafasi ya Everton ilikuwa mbaya kutokana na kushindwa
kutengeneza safu imara ya washambuliaji.
Walikuwa wa saba katika msimu wa 2010/11, lakini klabu 10 zilifunga mabao zaidi yao.
Walikuwa wa 11 msimu wa 2005/ 2006 na pia ni msimu ambao walifanya vibaya mno. Everton kwa sasa ipo nafasi ya sita na inaweza kumaliza hata nafasi ya saba.
Bado kuna maswali mengi, kwamba kweli Moyes ni kocha stahiki wa kumrithi Ferguson Manchester United?
Walikuwa wa 11 msimu wa 2005/ 2006 na pia ni msimu ambao walifanya vibaya mno. Everton kwa sasa ipo nafasi ya sita na inaweza kumaliza hata nafasi ya saba.
Bado kuna maswali mengi, kwamba kweli Moyes ni kocha stahiki wa kumrithi Ferguson Manchester United?
Kwa nini inasemekana Man United ni kama imepotea
kwa kuchagua jina la mtu ambaye nyota yake haijang’aa wakati kuna
makocha wenye majina makubwa Ulaya kama, Carlo Ancelotti aliyewahi
kuzinoa AC Milan, Juventus, Chelsea na Paris St-Germain?
Mwingine ni Mourinho aliyewahi kuzinoa Porto, Chelsea, Inter Milan na Real Madrid?
Ferguson ajibu
Hayo ni mawazo ya watu tu, lakini Alex Ferguson anaamini Moyes ana sifa zote za kuinoa Manchester United na siku zote alikuwa akimwaza kuwa ni mmoja wa makocha wanaoweza kumrithi. Ferguson alisema anatarajia makubwa kutoka kwa kocha huyo.
Mwingine ni Mourinho aliyewahi kuzinoa Porto, Chelsea, Inter Milan na Real Madrid?
Ferguson ajibu
Hayo ni mawazo ya watu tu, lakini Alex Ferguson anaamini Moyes ana sifa zote za kuinoa Manchester United na siku zote alikuwa akimwaza kuwa ni mmoja wa makocha wanaoweza kumrithi. Ferguson alisema anatarajia makubwa kutoka kwa kocha huyo.
“Wakati tulipojadiliana juu ya nani anaweza kazi
kwenye klabu hii, kila mtu alikiri Moyes ni mtu sahihi. Sidhani kama mtu
yeyote ana swali juu ya kiwango chake. Atawapeleka puta wapinzani
wake,” alisema.
Naye Mwenyekiti wa Everton, Bill Kenwright,
amekiri amempoteza kocha mahiri. Bill alisema kuwa kama angekuwa na
nguvu ya kumzuia angemzuia, lakini hana uwezo huo na akaongeza kuwa
amepata pigo kubwa.
Naye Moyes alisema anajiona mwenye bahati kuwa kocha mpya wa Manchester United.
Pia mkongwe wa Old Trafford, Sir Bobby Charlton, alisema David Moyes ni mashine mpya kwenye klabu hiyo. Mkurugenzi huyo aliongeza: “Nimewahi kusema nataka kocha mpya awe anaifahamu Man United. Moyes anafahamu cha kufanya.”
Pia mkongwe wa Old Trafford, Sir Bobby Charlton, alisema David Moyes ni mashine mpya kwenye klabu hiyo. Mkurugenzi huyo aliongeza: “Nimewahi kusema nataka kocha mpya awe anaifahamu Man United. Moyes anafahamu cha kufanya.”
Baada ya kukubali kutua katika klabu hiyo kwa
mkataba wa miaka sita Moyes alitamka: “Ni jambo la heshima kuona
Ferguson akinichagua, ninaheshimu kila kitu alichofanya. Itakuwa ni kazi
ngumu kufuata nyayo za kocha mzuri, lakini nitajitahidi.”
0 comments:
Post a Comment